Tuesday 17 March 2015

MOTO MWINGINE WAZUKA UDSM NA KUTEKETEZA OFISI YA DARUSO:

Baada ya kutokewa na ajali ya moto katika hostel za Mabibo, ofisi ya waziri mkuu DARUSO nayo ikawaka moto wakati waziri mkuu akiwa mabibo kushughulikia janga la moto lililotokea huko.
Chanzo cha habari yetu kimeeleza kuwa Naibu Spika wa bunge la DARUSO amesema kuwa moto huo inawezekena ukawa umesababishwa na shot ya umeme kwa sababu ofisi ilikuwa imefungwa na kulikuwa hakuna mtu.
Ifahamike kuwa ofisi hiyo iko mbali kabisa na hostel za mabibo na eneo jingine tofauti kabisa.
Chanzo cha habari kimesema kuwa moto huo ulianza mida ya saa tatu usiku.
"Nlikuwa MTU Wa kwanza kuanza kuuzima na kwa kushirikiana na Mbunge Tumsifu Robert  tukapta ushirikino toka kwa wakaazi Wa hall 6 na 7 tukiwa nje tukafanikiwa kuuzima moto baada ya kuvuja baadhi ya vioo katika office hiyo lakini ukweli ni kwamba tuwaachie wataalam waseme chanzo lakini nikifa leo niache ujumbe huu  "
Moto ule umesababishwa na sababu nyingine Nje na shoti ya umeme" alieleza shuhuda wa tukio hilo.

Kwa bahati nzuri moto ulidhibitiwa na hivyo ni makochi ya kukalia wageni tu ndiyo yaliyoungua na kuziacha document na kiti na meza ya Waziri Mkuu vikiwa salama.
Hili ni tukio la tatu kubwa ba labkusikitisha kwa UDSM, ikiwa ni pamoja na moto uliounguza hostel za Mabibo Block B na ajali ya gari ya Majinja iliyoua wanafunzi watano toka UDSM.